contact

husen

Saturday, July 13, 2013

MAONI : UVCCM wahimiza Serikali mbili tu

‘Uwapo wa Serikali tatu ni kuongeza gharama za uendeshaji na badala yake fedha hizo zinaweza kuelekezwa katika miradi ya maendeleo yenye tija kwa taifa.’ Katibu Mkuu wa UVCCM, Martine Shigela  
Na Ibrahim Yamola na Irene Mossi, Mwananchi  (email the author)

Kwa ufupi
  • Kauli hiyo ya UVCCM, inakwenda sambamba na ile ya Chama hicho iliyotolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye kuwa chama hicho bado kinaamini kuwapo kwa muungano wenye muundo wa Serikali mbili.

Kufuatia Rasimu ya Katiba,  iliyopendekeza muundo wa Serikali tatu zitakazojitegemea.
Dar es Salaam. Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM),imepinga mapendekezo ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya juu ya muundo wa Muungano kuwa wa Serikali tatu.
Katibu Mkuu wa UVCCM, Martine Shigela,akizungumza na waandishi wa habari jana alisema, kisheria muundo wa Serikali tatu hauna tija hususani kwa Watanganyika.
Alisema kilichotakiwa kabla ya tume kupendekeza uwapo wake, ilitakiwa kutoa mapendekezo ya Katiba tatu ya kila upande.
“Kama kweli tume walitaka kutuonyesha tunataka Muungano wa Serikali tatu, wangekuja na ‘Proposal’ mapendekezo ya Katiba ya Serikali zote lakini si hivi wanavyofanya,”alisema Shigela na kuongeza:
“Uwapo wa Serikali tatu ni kuongeza gharama za uendeshaji na badala yake fedha hizo zinaweza kuelekezwa katika miradi ya maendeleo yenye tija kwa taifa.”
Kauli hiyo ya UVCCM, inakwenda sambamba na ile ya Chama hicho iliyotolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye kuwa chama hicho bado kinaamini kuwapo kwa muungano wenye muundo wa Serikali mbili.
“Mapendekezo ambayo ndiyo msimamo wa chama tulishayawasilisha kwenye Tume kuwa sisi tunapendekeza mfumo wa Serikali mbili na siyo tatu wala moja,” alinukuliwa Nape alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Dodoma mwezi uliopita.
Shigela alisema kisheria haiingii akilini kuundwa kwa chombo cha Serikali tatu huku kukiwa na ukinzani juu ya katiba za nchi washirika.
“Tutakuwa na Katiba ya Muungano,Zanzibar wanayo ya kwao lakini Tanzania bara bado hawana Katiba hivyo kunatakiwa kila upande uwe na katiba yake kabla ya kupata Katiba ya Muungano,” alisema Shigela na kuongeza:
“Kupitia mawazo yatakayotolewa na vijana wetu kipi wanakitaka kuhusu Muungano wetu tutakichukua na kukipeleka katika ngazi ya juu kabla ya kukitolea ufafanuzi.”
Katibu Mkuu huyo alielezea kuwa umri wa kugombea Ubunge kupandishwa kutoka miaka 21 hadi 25 ni kuwanyima fursa vijana wengi kushika nafasi za uongozi.Alitolea mfano kuwa endapo mtoto ataanza darasa la kwanza akiwa na miaka saba, atahitimu Chuo Kikuu akiwa na umri wa miaka 23 hivyo kuwa na uwezo wa kushika nafasi ya kuongoza wananchi  hivyo pendekezo hilo bado halina tija kwani mtu akihitimu chuo anakuwa uwezo.

No comments:

Post a Comment