contact

husen

Wednesday, August 29, 2012

MIT ROMNEY KUPAMBANA NA OBAMA

 Mitt Romney ameteuliwa rasmi kama mgombea urais wa chama
 cha Republican katika kongamano la chama hicho huko Tampa, Florida.
Wajumbe kutoka majimbo yote ya Marekani walikusanyika
 kuthibitisha kumuunga mkono gavana huyo wa zamani
 wa jimbo la Massachusetts.
Atakabiliana na Barack Obama katika uchaguzi wa urais wa mwezi Novemba.
Kura ya maoni ya hivi karibuni inaonyesha wagombea hao
 wawili Bwana Romney na rais Obama wakipimana nguvu kwa karibu.
Bwana Romney, 65, alihitaji kupata japo kura za wajumbe
 1,144 ili aweze kuteuliwa kama mgombea wa chama chake,
na kura za kutoka jimbo la New Jersey zilimuweka "katika nafasi nzuri".
Dakika chache baadaye, mjumbe wa bunge la congress wa
Wisconsin Paul Ryan akateuliwa rasmi kuwa mgombea wa
 kiti cha makamu wa rais wa chama cha Republican.
Fursa ya Ann Romney
Bwana Romney aliteuliwa na wajumbe ambao walikuwa
 wakitangaza kura za majimbo yao kwa sauti hadharani.
Kwa ujumla, Bwana Romney alipata kura 2,061, Spika wa
 bunge la waakilishi John Boehner alitangaza katika kongamano hilo.

Bwana Romney hakuwepo kwenye kongamano hilo,
 lakini alifuatilia kuhesabiwa kwa kura akiwa katika
 hoteli ya karibu yeye na mkewe.
Uteuzi wake huko Tampa unathibitisha rasmi kuidhinishwa
 na chama chake kufanya kampeni.
Waliozungumza kwenye kongamano hilo walimshambulia rais Obama.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya chama cha
Republican Reince Priebus alisema rais hajawahi
 "kusimamia kampuni. Hajawahi hata kusimamia karakana."
Wakati huo huo, Bwana Boehner amesema:
  "utendaji kazi wa rais Obama si wa kiwango cha kusifiwa."
Siku ya Jumanne jioni, Ann Romney pia pamoja na Gavana
 wa jimbo la Carolina Kusini Nikki Haley na
 Gavana wa jimbo la New Jersey Chris Christie walizungumza
 
 

No comments:

Post a Comment