contact

husen

Saturday, September 8, 2012

WAPIGANAJI WA BOKO HARAM WAUAWA NCHINI NIGERIA

Jeshi la Nigeria linasema limewaua watu saba wanaoshukiwa
 kuwa wafuasi wa kundi la wapiganaji wa Kiisalmu wenye
 msimamo mkali la Boko Haram katika mapambano kaskazini mwa nchi hiyo.
Msemaji wa jeshi hilo amesema watu wengine zaidi kumi
 na watatu wamekamatwa baada ya kushambulia kituo cha
 ukaguzi cha jeshi, katika mji wa Maiduguri.
Ghasia hizo zimetokea siku moja baada ya polisi wa Nigeria,
kusema kuwa wataanza kulinda kutwa-kucha, milingoti
 ya simu za mkononi kufuatia milingoti kadhaa kama hiyo
 kushambuliwa mwezi uliopita, kaskazini mwa nchi.
Boko Haram ilisema ilifanya mashambulio hayo, kwa
 sababu milingoti hiyo inatumiwa kufuatilia
mawasilino baina ya wafuasi wake.
Akitoa maelezo ya tukio hilo la Maiduguri, Luteni Kanali
 Sagir Musa amesema, ''Kundi la watu wenye silaha
wanaoshukiwa kuwa wafuasi wa Boko Haram walishambulia
 kituo cha ukaguzi cha kijeshi sehemu ambayo wanajeshi
 walikuwa wameweka kizuizi na kufanya ukaguzi.
Ramani ya Nigeria ikionyesha eneo la Maiduguri

''Wanajeshi walijibu shambulio hilo kwa risasi. Watu saba wenye
 silaha waliuawa katika majibizano hayo ya ufyatulianaji risasi,
 na wengine kumi na watatu walikamatwa huku
 wengine wakikimbia. Hakuna majeruhi waliopatikana
 kwa upande wa wanajeshi.''
Boko Haram wanataka kuwekwa kwa utawala wa sheria
ya Kiislamu nchini Nigeria.
Kundi hilo lilianzisha kampeni ya kijeshi mwaka 2009
 kupigania kuanzishwa kwa utawala wa Kiislamu, likishambulia
 majengo ya serikali na makanisa na pia kuwaua wahubiri wa
 Kiislamu wenye msimamo wa kati.
Nchi hiyo imegawanyika kati ya eno la kaskazini lenye Waislamu
 wengi na lile la kusini linalokaliwa na Wakristo wengi na dini nyingine.
 
picha na stori kwa hisani ya bbc

No comments:

Post a Comment