contact

husen

Sunday, August 26, 2012

MWANA ANGA WA MAREKANI AFARIKI DUNIA

Neil Armstrong
Rais Obama ameongoza katika sifa na rambi-rambi zilizotolewa
 baada ya kifo cha Neil Armstrong, mwana anga wa kwanza kutua
 kwenye mwezi, ambaye amefariki akiwa na umri wa miaka 82
 kutokana na matatizo aliyopata baada ya upasuaji
 aliofanyiwa kwenye moyo.
 
Rais Obama alimuelezea Neil Armstrong kwamba ni mmoja
 kati ya mashujaa wakubwa wa Marekani, siyo wakati wake tu,
 lakini katika historia ya nchi hiyo piya.
Mwenzake Armstrong katika safari ya kihistoria ya kwenda
 mwezini mwaka wa 1969 alikuwa Buzz Aldrin, ambaye alisema
 Armstrong alikuwa rubani na kamanda mahiri.
Familia ya Neil Armstrong imetoa wito kwa Wamarekani kuonesha
 heshima zao kwa kufuata mfano wake wa kutumika
, kufanikiwa na bila ya majivuno.
Taarifa ya familia iliwaambia wale washabiki wake:
"ukitembea nje usiku ukaona mwezi unakuchekea,
 mfikirie Neil na umkonyeze."

picha na stori kwa hisani ya bbc

No comments:

Post a Comment